
Ludacris akiwa na Mwanadada Rosario Dawson wakati wa utoaji wa tuzo za MTV MOVIE AWARDS 2006
Nafikiri hili litakuwa somo kubwa sana kwa wasanii wa bongo na Afrika Mashariki kujitolea kwa mashabiki wao kiasi cha mapato wanachopata. Hiyo haimaanishi kuwa nao watoe magari 20 kama alivyofanya Ludacris ila wanaweza kutoa chochote kwa yatima, masikini wasiojiweza na wagonjwa wasio na msaada. Sidhani kama kweli watalalamika kuwa wanachopata ni kidogo hakiwezi kutosha kutoa msaada,si kweli kwa sababu starehe ambazo baadhi yao wanazifanya zinadhihirisha kuwa fedha ipo ingawa sio kivile. Kutoa msaada katika jamii ni njia nzuri sana ya kujitangaza na ni falsafa ya kisasa ambayo watu wengi wanaitumia kama Waingereza wanavyoita "Societo-Marketing philosophy". Kwa kufanya hivyo wasanii wa bongo na Afrika Mashariki wataheshimika sana na muziki wao utapendwa.
yes ni ukweli,lakini nawewe jiulize kwa nafasi yako ktk jamii unwasaidia wasiojiweza usije ukawa unapinga ufisadi wakati kumbe nawewe ni fisadi
ReplyDeleteOn my side,mimi sio employed and dats Why bado cjaweza kuwasaidia maskini na jamii ikanitambua but i promise to do so soon after gettg my first job appointment........ Lakini unataka kujifanya hujui kuwa huwa nakusaidia au mpaka niwape msaada watu wengine ndo ujue kuwa kweli nasaidia. Acha jeuri ukifulia ntakuwa sikutoi....Ha Ha Ha Am joking mjomba ila ukipata chochote wasaidie maskini!
ReplyDelete